‏ Psalms 1

KITABU CHA KWANZA

(Zaburi 1–41)

Furaha Ya Kweli

1 aHeri mtu yule ambaye
haendi katika shauri la watu waovu,
wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,
au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 bBali huifurahia sheria ya Bwana,
naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 cMtu huyo ni kama mti uliopandwa
kando ya vijito vya maji,
ambao huzaa matunda kwa majira yake
na majani yake hayanyauki.
Lolote afanyalo hufanikiwa.

Huzuni Ya Waovu

4 dSivyo walivyo waovu!
Wao ni kama makapi
yapeperushwayo na upepo.
5 eKwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,
wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

6Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki,
bali njia ya waovu itaangamia.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.