‏ Psalms 67

Mataifa Yahimizwa Kumsifu Mungu

Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.

1 aMungu aturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wake,
2 bili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.

3 cEe Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4 dMataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5 eEe Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.

6 fNdipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7 gMungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.