‏ Psalms 14

Uovu Wa Wanadamu

(Zaburi 53)

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 aMpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 b Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 cWote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!

4 dJe, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Bwana?
5Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 eNinyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
bali Bwana ndiye kimbilio lao.

7 fLaiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Bwana arejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.

Everyone uses cookies. We do too! Cookies are little bits of information stored on your computer which help us give you a better experience. You can find out more by reading the STEPBible cookie policy.