‏ Psalms 128

Thawabu Ya Kumtii Bwana

Wimbo wa kwenda juu.

1 aHeri ni wale wote wamchao Bwana,
waendao katika njia zake.
2 bUtakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 cMke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.
4 dHivyo ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Bwana.

5 e Bwana na akubariki kutoka Sayuni
siku zote za maisha yako,
na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 fnawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako.

Amani iwe juu ya Israeli.
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.