‏ Job 25

Bildadi Anasema: Mwanadamu Awezaje Kuwa Mwadilifu Mbele Za Mungu?

1 aNdipo Bildadi Mshuhi akajibu:

2 b“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3 cJe, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4 dMtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5 eIkiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6 fsembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”
Copyright information for SwhNEN
The selected Bible will not be clickable as it does not support the Vocabulary feature. The vocabulary is available by hovering over the verse number.